Alphonce Samambile Tambalu profile Pastor
Biography
Nimesoma shule ya msingi Ng'wakiyenze wilayani Misungwi Mwanza tangu 1975-1981 nilipohitimu nilijiunga na chuo cha Biblia cha Katungulu tangu 1987-1990 nilipohitimu. Nimekuwa mwinjilisti katika kanisa la AICT tangu 1990-1995 nilipoteuliwa kujiunga na chuo cha uchungaji kwa kuchukua kozi ya miezi mitatu katika fani ya Uchungaji huko Bwiru Mwanza ikiwa 1/6/1995. Niliwekewa mikono kuwa Mchungaji tarehe 28/1/1996 katika Pastorate ya AICT Bujora Mwanza. Nimekuwa katibu mkuu wa dayosisi ya Mwanza tangu 2005-2007. Baadae nilienda kusoma katika chuo cha Theologia cha Nassa Bulima, miaka minne tangu 2007-2011 nilipohitimi na kutunukiwa cheti cha Diploma ya juu na tangu 2011 hadi sasa ni katibu mkuu wa dayosisi ya Tabora. Nilimwamini Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wangu tarehe 10/4/1980 AICT Matale, Pastorate ya Sasi, Mwanza. Nilibatizwa tarehe 29/5/1982 katika maji ya mto Kisiwi huko Matale. Mchungaji aliyenibatiza ni Mch Jonathan Gwabo.